MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Friday 30 January 2015

RAIS MUGABE MWENYEKITI MPYA AU



RAIS mkongwe wa Zimbabwe Robert Mugabe, mwenye umri wa miaka tisini, sasa ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa muungano wa Afrika-AU.

Wajumbe walimteuwa Mugabe kwa kauli moja katika mkutano wa AU unaoendelea mjini Addis Ababa-Ethiopia.

Uteuzi wa Mugabe kuongoza muungano huo mkubwa ulio na wanachama zaidi ya arubaini, unaelezwa kuuingiza doa ndani ya AU, kwani Mugabe hana uhusiano mzuri na mataifa ya Magharibi, hasa baada ya kukaa uongozini tangu Zimbabwe ilipojipatia uhuru mnamo mwaka wa 80.

Miongoni mwa masuala  katika ajenda ni vita dhidi ya waasi  nchini Nigeria wa kundi la Boko Haram.

No comments:

Post a Comment