MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Friday 30 January 2015

UELEWA MDOGO WA WAZAZI KIKWAZO CHA ELIMU BORA KOROGWE



NA EVELYN BALOZI, KOROGWE
UELEWA mdogo kwa baadhi ya wazazi kuhusu umuhimu wa elimu umeelezwa kuwa janga la kukwamisha jitihada za serikali nchini kuwapatia elimu bora wanachi wake.

Afisa taaluma wa Korogwe Mji Elius Mavoa aliiarifu Jambo Leo juzi katika mahojiano maalumu juu ya hali ya elimu katika Halmashauri ya Wilaya hiyo yenye zaidi ya Shule za Msingi 133 na Shule za Sekondari 25 ambapo shule za Serikali 24 na jumuiya ya wazazi 1.

Inaarifiwa Mkurugenzi wa Korogwe Mji, Lewis Kalinjuna katika baraza la madiwani mwanzoni mwa juma aliagiza madiwani wa kata zote kuwaelimisha wazazi na walezi kuwahimiza watoto wao wazingatie masomo ili kujenga Taifa lenye wataalamu.

Na katika kuhakikisha hilo Mavoa alisema halmashauri hiyo imemeba jukumu la kuwasomesha zaidi ya wanafunzi 220 wa Sekondari na Msingi wanao ishi kwenye mazingira magumu.

Kati ya wanafunzi hao wanaosomeshwa, wa sekondari ni 120 na wa shule za msingi ni zaidi ya 100.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe Anjelus Bendera akifafanua zaidi alisema hatua hiyo imekuja baada ya Halmashauri kugugundua uwezo mdogo wa familia huchangia ongezeko la utoro kwa wanafunzi katika shule mbalimbali.

Alisema Halmashauri hiyo imeandaa mfuko maalumu kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi hao kupitia kitengo cha ukimwi na daftari la kuandikisha watoto wanao ishi kwenye mazingira magumu na hatarishi.

No comments:

Post a Comment