MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 29 May 2014

VIINI TETE KUZALISHIA NG'OMBE


  

 TAASISI ya mifugo kanda ya kati Taaliri inatarajia kuanza kutumia teknolojia  ya viini tete kuzalisha ng'ombe ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari  mkuu wa kitengo cha utafiti wa taasisi hiyo Geminius Tungu amesema kuwa mpango huo utatekelezwa kwa kushirikiana na tume ya sayansi na teknolojia  hapa nchini.

Tungu amesema  kuwa  uzalishaji wa viini tete ni teknolojia ya  ng'ombe mmoja kuweza  kuzalisha  mayai  matano hadi sita ambapo  ngombe huyo, atachomwa sindano  ya kukomaza mayai  mengi kwa wakati mmoja  na kuyarutubisha  kwa mbegu za dume na kuzipandikiza  kwa  ngombe wengine ambao watasaidia kulea  mimba  na muda ukifika    atazaa ndama wa kawaida.

Amesema uzalishaji huo  umelenga  kuchangia  na kumfanya mfugaji aweze kijitosheleza kwa chakula  na kuwa  na maendeleo ya kiuchumi  na kuongeza tija katika  mifugo  iliyopo  hapa nchini.

Mkuu huyo amefafanua kuwa teknolojia hii ikifanikiwa aidha Tanzania  itakuwa nchi ya kwanza  katika uzalishaji wa namana hii na itasaidia wafugaji kuwa na ng’ombe bora.

No comments:

Post a Comment