MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 29 May 2014

KAMATI YASEMA HAIRIDHISHWI UTEKELEZAJI KIGAMBONI


Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Mara na Mjumbe wa kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira


 KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira imesema hairidhishwi na mkakati wa utekelezaji wa Mradi wa Kigamboni.

Kamati hiyo imefikia hatua hiyo toka mchakato huo uanze kumekuwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na malalamaiko ya wakazi wa eneo husika .

Kauli hiyo imetolewa leo na  mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo Ester Bulaya alipokuwa akisoma taarifa ya kamati hiyo kwa kusema kumekuwa na malalmiko mengi toka kwa wananchi wa eneo hilo kuwa mchakato huo wa uandaaji wa mpango kabambe wa mji mpya haukuzingatia sheria ya mipango miji namba 8 ya mwaka 2007.

Ester Amesema mbali ya kutofuatwa kwa sheria hiyo pia wananchi wa eneo hilo walikatazwa kukarabati na kufanya shughuli za kimaendeleo katika maeneo yao huku utekelezaji wa mchakato huo kuwa wa muda mrefu kiasi cha kukatisha tama.

Amesema kutokana na changamoto hizo kamati yake inaitaka Serikali kuanza mara moja kukamilisha maandalizi ya mpango kabambe na kuanza utekelezaji wa mradi.

No comments:

Post a Comment