MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Wednesday 28 May 2014

HABARI ZA TANGA MAY 28, 2014

 ·    
Ramani ya Mkoa wa Tanga
 

    WAFANYA biashara wa mazoa ya nafaka na samaki waliopo barabara ya 15 Kata ya Ngamiani Kusini mijni hapa, wameiomba Halmashauri ya jiji la Tanga kusimamia usafi wa mifereji iliyopo kandokando ya barabara hiyo ambayo  imekuwa chanzo kikuu cha kuwepo kwa magonjwa ya milipuko pamoja mazalia ya mbu  hususani kipindi cha mvua.
Wakizungumza na Redio huruma ya Mkoani Tanga kwa nyakati  tofauti  Akida Ramadhani na Kimaro Gilioni wamesema wao wamekerwa na hali ya uchafu uliopo ndani ya mifereji  hiyo ambayo inasababisha maji machafu kutuama jambo amablo linahatirisha  afya wakazi wa eneo hilo.
Wafanya biashara hao wameiomba Halmashuri kuchua hatua  ya kusafisha mifereji hiyo ili maji yapite kwa uraisi badala ya wafanya biashara kuhangaika wenyewe kuwatafuta vibarua na kuwalipa wenyewe kwa muda mrefu.
Akilizungumzia suala hilo Mwenyekiti wa  Mtaa wa Jamhuri Kata ya Ngamiani Kusini, Shaban Choyo amesema kuwa  ni wajibu wa kila mfanya buiashara kusimamia usafi katika eneo hilo hali ambayo itasaidia  kuondokana na magonjwa ya mlipo kama Dengue na mengineyo.
Amesema yeye kwa kushirikiana na viongozi wengine wa kata watahamasisha jamii zaidi  juu ya usafi huo wa mifereji  kama wanavyo fanya katika maeneo mengine ikiwemo barabarani.


 ·       KATIKA TUKIO JINGINE
   WANANCHI wametakiwa kuwa makini na kuzingatia sheria za usalama barabrani ili kuepusha ajali zinazotokea mara kwa mara  mkoani hapa.
Akizungumza na radio huruma cha Mkoani Tanga leo katika kipindi cha tungumze asubuhi askari wa kikosi cha usalama wa barabarani PC IMANI mesema nivyema kila mwananchi atambue umuhimu wa kujua alama za vivuko wanapo kuwa barabarani. 
Amesema vivuko hivyo vya barabarani  ambavyo ni punda milia, vivuko vinavyoongozwa na taa za barabarani  na  vivuko vinavyoongozwa na askari wa polisi endapo vitafuatwa kwa usahihi kwa asilimia kubwa vinaweza kuondoa ajali za barabarani.
Sanjari na hayo ametoa rai kwa wananchi kushirikiana na jeshi la polisi katika kuwapa taarifa zinazo husu uvunjifu wa sheria  za barabarani.

No comments:

Post a Comment