MWANAMKE MAKINI BLOG

Advertise Here

Thursday 29 May 2014

65 MBARONI KUSHIRIKI UKAHABA

JESHI la Polisi mkoa wa Dodoma, limefanikiwa kukamata jumla ya wanawake 65 kwa kosa la kufanya biashara ya ukahaba katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.




Akizungumza na Blog hii mjini Dodoma  kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, kamishina msaidizi mwandamizi David Misime, amesema wanaweke 36 walikamatwa katika kipindi cha mwaka 2013 na wanawake wengine 29 walikamatwa mwaka 2014.



Kamanda Misime amesema kuwa wanawake hao walikamatwa katika mitaa mbalimbali ya mji wa Dodoma,wakifanya biashara ya kuuza miili yao hasa nyakati za usiku ambapo baadhi yao walitozwa faini na wengine walifungwa vifungo vya nje.



Kamanda Misime ametoa wito kwa wanawake wenye tabia hiyo kuacha mara moja ,huku akisisitiza kwamba Polisi wataendelea kuwakamata.

No comments:

Post a Comment